24.2 C
Dar es Salaam
Friday, October 18, 2024

Contact us: [email protected]

Mwaka 2030 upatikanaji maji safi kuwa 100%

Na Asha Bani, Dar es Salaam

Serikali imesema ifikapo 2030 upatikanaji wa maji safi na salama utakuwa wa asilimia mia moja.

Pia mpaka sasa miradi ya maji takribani 1,423 imekamilika
licha ya kuwa bado kuna baadhi ya maeneo yana changamoto za
upatikanaji wa maji hasa maeneo ya vijijini.

Hayo yameelezwa leo Desemba 3, na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Injinia Antony Sanga wakati alipokutana na wadau wa maji kutoka ndani na nje ya nchi, ambapo amesema mpaka sasa serikali imefanya kazi ya kuhakikisha maeneo mengi nchini yanakuwa na maji safi na salama ya uhakika.

Injinia Sanga amesema kuwa miradi mingi imekaqmilika na kwamba
upatikanaji wa maji katika meneo ya vijijini ni kwa asilimia 70 huku
maeneo ya mijini ni kwa asilimia 80 huku lengo ikifika 2030 kuwepo na
upatikanaji wa maji sawa kwa asilimia 100.

“Katika uongozi wa Rais Dk. John Magufuli tumepambana na kuhakikisha maji
kwa asilimia kubwa yanapatikana licha ya kwamba kuna changamoto ndogondogo ambazo tunahakikisha ifikapo 2030 kila kitu kitakuwa sawa,’’ amesema.
Naye Mwenyekiti wa jukwaa la watumiaji wa maji Injinia Mbogo Futakamba alisema hali ya usambazaji wa m,aji nchini unaridhisha licha ya kwamba kuna maeneo bado yanaupotevu wa maji.

Amesema kwa sasa udhibiti wa upotevu wa maji upo kwa asilimia 30 mapaka 35 lakini lengo ushuke mpaka kufikia asilimian 20 mapaka 25.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
590,000SubscribersSubscribe

Latest Articles