MERSEYSIDE, England
LIVERPOOL wameanza kusuka mpango wa kuibomoa Chelsea kwa kumchukua mshambuliaji wake raia wa Marekani, Christian Pulisic.
Liverpool wanataka Purisic atue Anfield kupitia dirisha dogo la usajili (Januari, mwakani), wakifahamu kuwa mchezaji huyo hana nafasi ya kucheza Stamford Bridge.
Tayari tetesi za kuikimbia Chelsea zimekuwa nyingi, ikiwamo ile inayomuhuisha na vigogo wa Catalunya, Barcelona.
Kile kinachoonekana kuipa nguvu zaidi Liverpool ni uhusiano wa Pulisic na kocha wao, Jurgen Klopp, kwa waliwahi kuwa pamoja Borussia Dortmund.