24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Koeman atia aibu Barca

MADRID, Hispania

RONALD Koeman amekuwa kocha wa kwanza wa Barcelona ndani ya miaka 81 kupoteza El Clasico zote tatu za mwanzoni mwa kibarua chake.

Mholanzi huyo aliweka rekodi mbovu hiyo jana baada ya Barca kutandikwa mabao 2-1 na wapinzani wao wakubwa, Real Madrid, mchezo uliochezwa Camp Nou.

Sergio Aguero aliitanguliza Barca lakini mabao ya David Alaba na Lucas Vazquez yalitosha kuifanya Madrid iondoke na pointi tatu za ugenini.

Ukiacha Koeman, kocha mwingine aliyewahi kufungwa mara tatu na Madrid mwanzoni mwa kibarua chake ni Patrick O’Connell aliyeinoa Barca kuanzia mwaka 1935 hadi 1940.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles