30.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Kane, Conte kupishana Spurs

LONDON, England

IMEFICHUKA kuwa straika wa Tottenham, Harry Kane, anajiandaa kuondoka zake baada ya klabu hiyo kumwajiri kocha mpya, Antonio Conte.

Wakati huo huo, Conte anatazamiwa kuanza na kiungo wa AC Milan, Franck Kessie, katika harakati za kukisuka kikosi cha Tottenham.

Hayo yanasemwa huku Kane akisema Conte ni mmoja kati ya makocha bora duniani, ikiwa ni mara ya kwanza kwa mchezaji huyo kuzungumza tangu Tottenham ilipomtimua Nuno Espirito Santo.

Mfungaji bora huyo wa Ligi Kuu England msimu uliopita, alikaribia kujiunga na Manchester City miezi michache iliyopita, kabla ya Mwenyekiti wa Tottenham, Daniel Levy, kuzuia biashara hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles