27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Irene Uwoya awataka wasanii kujiingiza kwenye biashara

ireneeeNA THERESIA GASPER

MKALI wa filamu nchini, Irene Uwoya, amewataka wasanii wenzake hasa wanawake kujituma katika kazi nyingine kama vile biashara ili kuweza kujikomboa kimaisha.

Irene amesema wasanii wengi wanategemea sanaa ili kuweza kuendesha maisha yao, lakini wanatakiwa kufanya mambo mengi ili kuweza kujiingizia kipato.

Akizungumza na MTANZANIA jana alisema yeye ana ofisi ambayo inajishughulisha na ushonaji wa nguo za aina zote ambayo inamsaidia kuingiza kipato na huwa anashona.

“Natumia kauli mbiu ya hapa kazi tu kwani mtu huwezi ukategemea kitu kimoja na hasa sisi wasanii huwezi ukategemea sanaa lazima utafute kitu kingine ambacho kitaweza kukusaidia,” alisema.

Alisema ni vema mtu akajiongeza katika kazi yenye uhalali ili aweze kufanya vitu vya msingi ambavyo vitamfanya kuendesha maisha yake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles