MAONYESHO ya kipekee ya Harusi Trade Fair 2016 yanatarajiwa kufanyika kuanzia Machi 11 mwaka huu katika Ukumbi wa Cardinal Rugambwa, uliopo karibu na Kanisa la St. Peter, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Ofisa mradi huo, Hurbert Kisasi, alisema maonyesho hayo yanayoandaliwa na mwanamitindo, Mustafa Hassanali, yamevutia waonyeshaji bidhaa mbalimbali za harusi kutokana na ubunifu wake.
Mratibu wa maonyesho hayo, Naomi Godwin, alisema hakutakuwa na kiingilio hivyo wadau mbalimbali wajitokeze kwa wingi.