23.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Hans Poppe awabeza Yanga

Hans PoppeNA MWALI IBRAHIM, DAR ES SALAAM
MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya klabu ya Simba, Zacharia Hans Poppe, amewabeza wapinzani wao Yanga akidai kuwa kipigo walichokipata kutoka kwa timu waliyoidharau kimewaumbua.
Simba ndio walikuwa wenyeji wa mchezo huo wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL) uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ambapo Yanga ilikubali kipigo cha bao 1-0.
Akizungumza na MTANZANIA mara baada ya kumalizika mchezo huo, Hans Poppe alisema maneno mengi yalisemwa juu ya kikosi cha Simba kuwa hakina uwezo wa kuifunga Yanga, lakini kilichotokea kila mmoja alishuhudia.
“Tuliambiwa sisi sio wapinzani wa Yanga kwa kuwa wanashindana na timu za kimataifa tuliona ni sawa, lakini kipigo kimewaumbua na kudhihirisha kuwa sisi ni bora na hawawezi kutufunga,” alisema.
Alisema timu hiyo sasa inajipanga kusaka matokeo ya ushindi katika mechi zilizobaki Ligi Kuu ambapo Jumamosi ijayo watakutana na Mtibwa Sugar.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles