MUNICH, Ujerumani
MPACHIKAJI mabao hatari wa Borussia Dortmund, Erling Braut Haaland, anataka kuikacha klabu hiyo wakati wa usajili wa kiangazi, mwakani.
Haaland (21), ameshaingia kambani mara 70 katika mechi 69 tangu aliposajiliwa na Dortmund mwanzoni mwa mwaka jana akitokea RB Salzburg ya Ligi Kuu nchini Austria.
Hii ya kutaka kuondoka Dortmund inakwenda kuwa habari njema kwa mabosi wa klabu za Bayern Munich, Real Madrid na Manchester City, ambao mara kadhaa wamekuwa wakijaribu kuinasa saini yake.
Kwa upande mwingine, wakala wake anataka mchezaji huyo wa kimataifa wa Norway atue Barcelona.