MILAN, Italia
KIUNGO wa Inter Milan, Christian Eriksen, yuko tayari kurudi Ajax kwa kuwa sheria za soka la Italia hazimruhusu kucheza.
Eriksen amewekewa kifaa cha kusaidia mapigo ya moyo, jambo ambalo linamfanya asiruhusiwe kucheza Serie A.
Aidha, lejendari wa Tottenham, Fabrice Muamba, amemshauri Eriksen kuachana na soka kabisa kutokana na tatizo hilo la moyo.
Kama ilivyokea kwa Eriksen katika moja ya mechi za fainali za Euro 2020, pia Muamba aliwahi kuanguka uwanjani kutokana na changamoto hiyo.
“Kujihusisha na mchezo mgumu kama soka ni hatari pia kwa sababu mapigo ya moyo yanapanda na kushuka, si nzuri kwa moyo,” amesema Muamba.