27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Djockovic atwaa ubingwa wa US Open

KUBWANEW YORK, MAREKANI

NYOTA namba moja kwa ubora duniani katika mchezo wa tenisi, Novak Djockovic, amefanikiwa kuchukua ubingwa wa wazi nchini Marekani baada ya kumchapa mpinzani wake, Rodger Federer, anayeshika nafasi ya pili kwa ubora duniani.

Novak amemshinda Federer kwa jumla ya seti 6-4 5-7 6-4 6-4, kutokana na ushindi huu mchezaji huyo jumla atakuwa ametwaa mataji matatu ya Grand Slam mwaka huu.

Mbali na kuchukua mataji matatu mwaka huu, mchezaji huyo hilo litakuwa ni taji lake la 10 la Grand slam tangu aanze kucheza mchezo huo.

Kwa upande wa wachezaji wawili wawili, Martina Hingis na Sania Mirza, wametwaa ubingwa wa michuano hiyo baada ya kuwashinda wapinzani wao, Yaroslava Shvedova na Casey Dellacqua kwa seti 6-3, 6-3.

Ushindi huu ni wa nne kwa mwaka huu kwa wachezaji hawa, huku ukiwa ni ushindi wao wa pili wa Grand Slam.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles