NA MWANDISHI WETU
MWIMBAJI nguli wa muziki wa Injili, Bonny Mwaitege, ametoa wito kwa Watanzania kulipa uzito wa aina yake Tamasha la Pasaka kwa kujitokeza kwa wingi kuhudhuria tukio hilo adhimu.
Mwaitege alisema kupitia tamasha hilo jamii inaondokana na machafu yanayomchukiza Mungu.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama, alisema tamasha la mwaka huu wamejipanga vilivyo kufanikisha matakwa ya jamii kutoka kwa waimbaji wa nyimbo za injili na viongozi wa dini watakaohudhuria tamasha hilo.
Msama alisema tamasha la mwaka huu wamepanga lianze Machi 26 hadi 28 hapa nchini.