27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

AUNT EZEKIEL: HUU NDIO WAKATI WANGU WA KUPATA WATOTO ZAIDI

Na JESSCA NANGAWE – DAR ES SALAAM


MSANII wa filamu za Bongo, Aunt Ezekiel, amedai kwamba anatamani kupata watoto zaidi kwa kuwa huu ndio wakati wake wa kufanya hivyo na hajui atapata watoto wangapi katika maisha yake.

Aunt Ezekiel ambaye yupo kwenye uhusiano na dansa wa msanii Diamond Platnumz, Mose Iyobo, amesema kwa kuwa ndio wakati wake wa kufanya maamuzi sahihi na haoni idadi kamili ya watoto atakaokuwa nao katika familia yake na Iyobo.

“Nilitamani kuitwa mama sasa naitwa mama, naomba Mungu anisaidie nikuze familia yangu na anibariki nipate watoto wengine kwa kuwa watoto ndiyo furaha yangu zaidi,” alisema Aunt Ezekiel mwenye mtoto anayeitwa Cookie.

“Mtoto wangu wa pili natamani awe wa kiume na wengine zaidi ambao hata sijui watakua wangapi watakaokuwa na jinsia yoyote nitafurahi kwa kuwa tamaa yangu ni kuwa na watoto wengi,” alisisitiza.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles