27.5 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Aslay kupamba Krismas Musoma

Na Mwandishi Wetu, Musoma

Msanii wa Bongo Fleva, Aslay Isihaka ‘Aslay’ anatarajia kuwaburudisha wakazi wa mji wa Musoma siku ya Krismas Desemba 25, katika ukumbi wa Le Grand Beach.

Akizungumza na Mtanzaniadigital, Mratibu wa tamasha hilo lililopewa jina la ‘Shangwe za Christmas’, Shomari Binda, amesema maandalizi yote yamekamilika na kilichobaki ni wakazi wa Musoma kusubiri burudani.

“Aslay ameahidi kutoa burudani ya nyimbo zake zote kali na kuwaomba wakazi wa Musoma na vitongoji vyake kujitokeza kwa wingi kupata burudani ambayo haijawahi kutokea kabla,” amesema Binda.

Aidha, Binda amesema tamasha hilo litaambatana na muziki wa wa vyombo ‘Live band’ utakaopigwa na bendi ya New Le Grand Band.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles