24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

RITA yatakiwa kuendeleza uaminifu

Na Asha Bani,Dar es salaam

Waziri wa Katiba na Sheria, Mwigulu Nchemba amewataka Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) kuendeleza uaminifu ili kuepuka kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watu wasio raia wa Tanzania.

Hayo ameyasema leo Jumatatu Desemba 21, jijini Dar es Salaam alipokutana na uongozi was RITA na wafanyakazi kujadili mambo mbalimbali ya taasisi hiyo.

Amesema taasisi hiyo inaumuhimu mkubwa kwa serikali katika kupanga mambo yake na kuwataka kuongeza nguvu katika mfumo wa taarifa na namna ya kurathimisha taarifa hizo.

Wakati huo huo Naibu Waziri wa wizara hiyo Geofrey Pinda alisema baadhi ya sheria za mirathi zinatakiwa kufanyiwa marekebisho ili kuendana na uhalisia na wahusika kupata haki zao kwa muda muafaka.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles