33.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Wonderland ndani ya Maasai Festival

Na Elias Simon, Dar es Salaam

Kampuni ya Kitanzania iliyolenga kukuza utalii ndani ya Tanzania “Wonderland” leo tarehe 10 Disemba 2019. Imezinduwa Tamasha jipya liitwalo Masaai Festival, ambalo linatarajia kufanyika mwanzo wa mwaka 2020.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Said Maulid alisema wameandaa tamasha la maasai festival kwa lengo la kutoa mchango mkubwa kwenye swala la zima la utalii na pia juu ya maendeleo  ndani ya sekta hiyo ya utalii.

 “Wonderful imeandaa ili tamasha la masaai festival  kwa lengo zima la kukuza utalii na kutoa mchango juu ya swala zima la utalii ndani ya Tanzania” Alisema Said Maulid.

Kwa upande mwingine Mkurugenzi wa Kampuni hiyo ya Wonderland alichukuwa nafasi hiyo kuwatambulisha mabalozi ambao wataenda kushiriakiana nao kwa lengo la kulitangaza tamasha hilo la masaai festival.

Ndani ya mabalozi hao wapo wasanii wa mziki kama G nako kutoka kundi la weusi, Mrisho Mpoto (mjomba), mwigizaji batuli na wengine wengi.

Moja kati ya mabalozi  waliopata fursa ya kuongea na waanadishi wa habari ni G nako alisema “Hiki ni kitu kikubwa na tumeungana kama watanzania kutangaza utalii wetu kama”.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles