Jessca Victor, TUDARCo
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe, amesema sanaa ni biashara kubwa na endapo wasanii watashirikiana na Serikali sekta hiyo itazidi kukua
Kihage amezungumza hayo wakati akihutubia katika mkutano mkuu wa sekta ya sanaa ambapo wadau na wasanii wamewasilisha changamoto zao kama vile bidhaa zinazotumiwa na wasanii kuwa na bei ambayo sio rafiki.
Amesema lengo la mkutano huo ni kujadili sekta ya sanaa kati ya serikali na wadau ili kufikia malengo ya kufanya sekta hiyo kuendeshwa kibiashara na kuleta tija.
“Wasanii ni masoko ya kutoka viwandani na pia ni wahamasishaji wa biashara mbalimbali kwa hutumika hata katika matangazo makubwa ya biashara nchini Tanzania na ulimwenguni kiujumla.
“Wizara ya Viwanda na Biashara ni mdau mkubwa wa Wizara ya Sanaa na Utamaduni na Michezo, kwani sekta ya sanaa ni kiwanda kinachozalisha huduma za sanaa ambazo zinahitaji mchango mkubwa wa wizara,” amesema.
Ameeleza kuwa mipango ya Serikali ni kuweka mazingira wezeshi katika kukuza sanaa zetu ili kufikia kiwango cha Kimataifa, kuboresha mbinu za kimkakati ya utekelezaji wa sera na sheria za kurasimisha kazi na sanaa nchini na kuwashirikisha wadau mbalimbali wa sanaa hususani wasanii.