21.5 C
Dar es Salaam
Saturday, July 27, 2024

Contact us: [email protected]

Waziri Ummy atoa msaada wa mifuko 600 ya Saruji Tanga

Na Amina Omari, Tanga

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Ummy Mwalimu ametoa msaada wa mifuko 600 ya saruji yenye thamani ya Sh milioni 8.4 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za sekondari zilizopo kwenye Halimashauri ya Jiji la Tanga.

Msaada huo ametoa jana Desemba 27, baada ya kufanya ziara katika shule za tisa za sekondari ambazo zinatarajia kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwezi Januari 2021 ilo kujionea hatua za utekelezaji wa ujenzi huo

Ummy amesema kuwa ameridhishwa na kasi ya ujenzi huo inayofanywa na Halimashauri kwa kushirikiana na wananchi ili kuhakikisha lengo la serikali la wanafunzi wote waliofaulu kwenda kidato cha kwanza wanaanza masomo kwa wakati.

“Kama mbunge nimefurahishwa na juhudi zinazofanywa na wananchi katika kusaidia Serikali yao lakini katika kuweka mazingira wezeshi ya watoto wao kupata elimu, niwaahidi kusaidia juhudi hizo kwa hali na mali,” amesema Ummy.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles