23.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

WAZIRI LUKUVI ATANGAZA KIAMA WADAIWA SUGU ARDHI

Na MASYENENE DAMIAN -MWANZA

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, amesema ifikapo Aprili 30, mwaka huu ndiyo siku ya mwisho wa ulipaji kodi ya pango la ardhi kwa halmashauri zote nchini na wamiliki wa ardhi.

Lukuvi alisema wale wote watakaoshindwa kufanya hivyo watatangazwa kwenye magazeti ya umma na kuwasilisha taarifa zao kwa Rais Dk. John Magufuli ili awashughulikie.

Waziri Lukuvi alitoa agizo hilo wilayani Ilemela Mkoa wa Mwanza jana wakati akizungumza na wafanyakazi wa idara ya ardhi na watumishi wa manispaa hiyo katika ziara yake ya siku tatu ya kutatua migogoro baina ya wananchi na taasisi za Serikali.

Akizungumzia juu ya makusanyo ya kodi ya pango, Lukuvi, alizitaka halmashauri zote nchini kuhakikisha kuwa inalifanya zoezi la ukusanyaji wa kodi hiyo kuwa ya msingi na wajibu kwao na zifikie lengo la asilimia 100 za makusanyo ya mwaka wa fedha 2017/18 ifikapo Aprili 30, mwaka huu.

“Wasiofikia lengo hilo nitawatangaza kwenye magazeti ya umma na kupeleka taarifa zao kwa Rais aone wanavyomhujumu, tunafanya hii yote kwa sababu hii ni kodi pekee inayokusanywa na halmashauri kwa niaba ya Serikali kuu.

“Wale wote ambao hawajalipa (wadaiwa sugu), nataka kusikia mpaka kufikia mwezi wa tano wawe wamesekwa rumande kwa sababu tunataka mpaka kufikia mwisho wa mwaka wale wote waliotakiwa kulipa wawe wamelipa na mabaraza yote ya ardhi yawe bize kusikiliza mashauri haya ya ardhi, tutawaburuza mahakamani bila kujali jina na heshima zao,” alisema Lukuvi.

Hata hivyo, akizungumzia zoezi la urasimishaji katika wilaya za Ilemela na Nyamagana mkoani Mwanza, Waziri Lukuvi, aliwasifu kwa kazi nzuri waliyofanya huku akiwataka kuongeza kasi katika umilikishwaji wa ardhi.

 

 

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles