24.2 C
Dar es Salaam
Monday, May 6, 2024

Contact us: [email protected]

Watoto kumkamua Rick Ross mil 25

NGULI wa muziki wa Hip hop, Rick Ross, amekubali kulipa fedha za matunzo ya watoto wake watatu wanaoishi na mpenzi wake wa zamani, Briana Singleton.

Kwa mujibu wa kile kilichoelezwa na mtandao wa udaku wa TMZ, sasa Ross atalazimika kumpatia bibiye huyo Dola 11,000 (zaidi ya Sh mil. 25 za Tanzania) kila mwezi.

Wakati hicho kikionekana ni kiasi kikubwa cha fedha, bado kuna mzigo mzito kwa msanii huyo, kugharamia bima ya afya kwa watoto hao.

Imekuwapo misuguano kati yao tangu walipoachana, ikikumbukwa namna bibiye Briana alivyomzuia Ross kuwaona watoto, akisema aanze kupata chanjo ya Corona kabla ya kufika nyumbani kwake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles