25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Washindi 12 wa NMB MastaBata wapatikana

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Washindi 12 wa droo ya nane ya NMB MastaBATA, jana wamepatikana na kujizolea zawadi zenye thamani ya Sh milioni 28.8 hivyo kufanya zawadi zilizotolewa kufikia thamani ya Sh milioni 87.6 kati ya zaidi ya Sh milioni 200 zinazoshindaniwa.

Masoud Kipanya akizungumza na mmoja wa washindi wa Droo ya nane ya Promosheni ya Mastabata iliyochezeshwa jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkuu wa Biashara ya Kadi wa Benki ya NMB, Philbert Casmir na kushoto ni msimamizi kutoka Bodi ya Michezo ya kubahatisha, Upendo Albert

NMB MastaBATA inayoendeshwa na Benki ya NMB, ni kampeni inayolenga kuhamasisha matumizi na manunuzi kwa Kadi za NMB Mastercard na Masterpass QR, ilianza Novemba 24, mwaka jana, ikitoa zawadi za Sh 100,000 kwa washindi 40 kila wiki na washindi 12 wa Sh milioni 2.4 kila mwezi.

Akizungumza wakati wa droo hiyo ambayo ni ya pili kati ya tatu za mwezi, Mkuu wa Biashara ya Kadi wa NMB, Philbert Casmir, amesema katika droo saba zilizotangulia (sita za wiki na mbili za mwezi), zimewawezesha washindi wapatao 304 kujizolea zawadi za Sh milioni 87.6.

Casmir amebainisha kuwa, NMB MastaBATA imebakisha droo tatu kukamilisha miezi mitatu ya kampeni hiyo, ambayo zawadi kuu ‘Grand Finale’ itakuwa ni ziara ya utalii Zanzibar, Ngorongoro ama Serengeti, iliyolipiwa kila kitu na benki ya NMB, ambako washindi watakuwa huru kuchagua zawadi mbadala.

“Wito wetu kwa wateja wa NMB kuendelea kufanya matumizi na manunuzi mbalimbali kwa Kadi za NMB Mastercard na Masterpass QR, ili kujiongezea nafasi sio tu ya kushinda zawadi za wiki na mwezi, bali ziara hii ya kitalii katika moja kati ya maeneo hayo matatu,” amesema Casmir.

Katika droo ya jana, iliyofanyika chini ya usimamizi wa Ofisa kutoka Bodi ya Michezo Kubahatisha Tanzania (GBT), Pendo Albert, washindi 12 walikuwa huru kuchagua zawadi zilizogawanywa katika makundi matatu, kila moja likiwa na zawadi zenye thamani ya Sh milioni 2.4.

Katika kundi la kwanza kulikuwa na zawadi ya simu ya Samsung Galaxy Note20 yenye thamani ya Sh milioni 2.4, kundi la pili friji dogo, water dispenser, Microwave na Samsung A21 kwa pamoja. Kundi la tatu ni runinga (flat screen inchi 40) iliyolipiwa DSTV miezi mitatu, laptop na Samsung A21.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles