24.5 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Wapatanishi wa China wapuuza kitisho cha Trump

BEIJING, CHINA

SERIKALI ya China imesema bado inapanga kutuma ujumbe wake Marekani kufanya mazungumzo ya  biashara licha ya tishio la Rais wa taifa hilo, Donald Trump.

Trump aliapa kuongeza kodi za bidhaa kutoka China baadaye wiki hii, kitisho ambacho kimeathiri masoko ya hisa.

Trump alitoa kitisho hicho wakati wajumbe wa pande zote mbili wakijiandaa kukutana   Washington kesho kwa kile kinachoonekana kuwa duru la mwisho la mazungumzo ya kufikia muafaka ama afufue upya vita ya  biashara.

Trump amesema kodi ya bidhaa za China za thamani ya dola bilioni 200 zitapandishwa kutoka asilimia 10 hadi 25 Ijumaa wiki hii.

Licha ya hayo, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa China, Geng Shuang amesema timu yao kwa sasa inajiandaa kwenda Marekani kushiriki mazungumzo lakini hajaeleza kama mjumbe mkuu wa timu hiyo Liu He atauongoza ujumbe huo au la.

Geng amesema hatua nzuri  imepigwa katika duru 10 za mazungumzo ya ngazi ya juu yaliyofanyika na kuwa dunia nzima unafuatilia.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles