27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

AU yaunga mkono serikali ya kiraia Sudan

Umoja wa Afrika (AU) pamoja na Umoja wa Mataifa (UN) wanaunga mkono serikali ya kiraia nchini Sudan baada ya kupinduliwa madarakani kwa rais Omar al-Bashir mwezi uliopita.

Katika mkutano na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa halmashauri kuu ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat, amesema kwamba hatua ya baraza la jeshi kuendelea kuongoza nchi hiyo ni jambo lisilokubalika.

Mahamat ameyasema hayo baada ya kukutana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres. Mkuu huyo wa Umoja wa Afrika lakini amesema kwamba wanajeshi wanaweza kuwa sehemu ya serikali ya kiraia.

Waandamanaji wameendelea kushinikiza kwamba wanataka serikali ya kiraia na Umoja wa Afrika awali ulilipa jeshi la Sudan muda wa mwisho wa siku kumi na tano kupeana madaraka kwa raia, ingawa muda huo uliongezwa hadi siku sitini.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles