23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Wananchi Bukoba watakiwa kuanzisha miradi

Renatha Kipaka, Bukoba

Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera, wameshauri kuhimiza wananchi kujitoa katika kuchangia uanzishaji wa miradi ya maendeleo badala ya kutegemea Serikali pekee.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi​ wa halmashauri hiyo, Waziri Msafiri wakati akijibu​ taarifa za miradi ya maendeleo kwa mwezi Aprili hadi Juni mwaka huu​ zilizokuwa zikiwasishwa kutoka kwenye kata mbalimbali zikigusia  afya, barabara,elimu na ulinzi.

Msafiri amesema endapo madiwani wataongeza jitihada za kuhimiza wananchi kutenga maeneo na kuanzisha uwekaji wa maboma​ kama sehemu ya miradi ya maendeleo kwa kutegemea Serikali kukamilisha.

“Niwashauri madiwani​ kuweni na viwanja vya kujenga maboma kwenye maeneo ya wananchi pia waanzishe ili Serikali inapoombwa hela tuwe na maeneo ya kuonyesha jitihada zilizokwisha fanywa”amesema Msafiri

Diwani wa kata Kagondo Joram Ifunya, amesema katika kata hiyo kuna ukosefu wa zahanati ya kliniki ya mama na mtoto hali inayofanya usumbufu kwa jamii.

Amesema jamii inayoishi katika kata hiyo inatumia huduma ya kliniki Tembezi ambayo inamfuata  alipo na kuna tatizo la utimilifunwa huduma hiyo.

Diwani wa kata Nshambya​ Meya wa Manispaa hiyo, Godson Rumanyika, amesema licha yakuwepo na uhaba wa zahanati kwa kila kata bado kuna tatizo la wahudumu wa afya ambao watahitajika kutoa huduma kwa jamii.

Amesema tayari kiasi cha sh.milioni 500 kimepangiwa kujenga hospitali ya Manispaa ya Bukoba licha ya kupambana na kuweka zahati kila kata

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles