27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Wakazi Dar: Tusipolipa tozo tunachelewesha maendeleo yetu

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wameendelea kutoa maoni juu ya Tozo za Miamala ya Simu na Benki kufuatia ufafanuzi wa Serikali uliotolewa na Waziri wa Fedha na Mipango, pamoja na Mawaziri wengine

Wakizungumza na Mtanzania Digital kwa nyakati tofauti wengi wa wakazi hao wameeleza kuwa, hawakuwa wakijua kinagaubaga Tozo hizi zinatumikaje lakini baada ya Ufafanuzi uliotolewa, wako tayari kulipa Tozo kama mchango wao katika maendeleo ya Taifa letu

Aidha, wakazi hao wa Jiji la Dar es Salaam, wametoa wito kwa Wananchi wengine kulipa Tozo kwani Serikali inategemea Tozo hizo katika kuliletea Taifa maendeleo, na kama tutakuwa waziro katika ulipaji wa Tozo tutakuwa tunachelewesha maendeleo yetu wenyewe.

“Tozo ni muhimu katika kuchochea maendeleo na kuboresha huduma za kijamii, tuko tayari kulipa tozo na tunatambua umuhimu wake katika maendeleo ya taifa letu, katika hili tyunamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan.

“Tunaona faida zake ikiwamo vituo vya afya, barabara na huduma nyingine kama sababu zinazotupa msukumo wa kuchangia kidogo kupitia tozo zilizowekwa na Serikali yetu ili kuharakisha upatikanaji wa huduma hizo kote nchini,” wameeleza wakazi hao.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles