31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Wagonjwa Muhimbili wasotea huduma ya CT -Scan

Hadia Khamis na Johanes Respichius (RCT), Dar es Salaam
BAADHI ya wagonjwa wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), wamelalamikia hatua ya uongozi wa hospitali hiyo kushindwa kuchukua hatua za dharura za kutoa huduma za CT-Scan, ambayo imeharibika kwa kipindi cha miezi miwili sasa.
Wakizungumza na MTANZANIA kwa nyakati tofauti, wagonjwa hao walisema wamekuwa wakiteseka kwa kipindi cha miezi miwili sasa bila kupata huduma hiyo.
Mmoja wa wagonjwa hao aliyejitambulisha kwa jina la Rashid Omari, alisema ni mwezi wa pili sasa amekuwa akienda na kurudi hospitalini hapo bila ya kupata huduma.
“Kila nikifika bado nakutana na bango la ujumbe unaosomeka mashine ni mbovu mafundi wanafanya matengenezo, nimekuwa nikienda na kurudi huku tatizo likizidi kukuwa, mpaka sasa sijui hatima yangu itakuwaje,” alisema Omari.
Akizungumza na MTANZANIA Ofisa Uhusiano wa Hospitali hiyo, Aminiel Eligaesha, alikiri kuharibika kwa mashine hiyo na kusisitiza kuwa tayari uongozi umeshaagiza kifaa cha mashine hiyo kutoka nchini Afrika Kusini.
“Tunatarajia kifaa hicho kitafika haraka iwezekanavyo ili kuweza kuwapatia huduma ya kipimo cha CT-Scan wagonjwa wetu wanaokuja kwa ajili ya kufanyiwa kipimo hicho,” alisema Eligaesha.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles