23.9 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

vipodozi feki yakamatwa

3TUNU NASSOR NA RUTH MNKENI, DAR ES SALAAM

MAMLAKA ya Chakula na Dawa (TFDA), imekamata shehena ya vipodozi tani 12 vilivyopigwa marufuku katika majengo mawili ya ghorofa tatu yaliyopo Mtaa wa Jangwani, Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Pia imewakamata waagizaji na wasambazaji wakubwa 24 wa bidhaa hizo wanaodaiwa pia kuwa wanahifadhi bidhaa zao katika majengo hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamata shehena hiyo, Meneja wa Kanda ya Mashariki wa TFDA, Emmanuel Alphonce, alisema msako huo ulianza juzi na kufanikiwa kukamata jengo moja la ghorofa tatu huku mbili zikiwa zimejaa vipodozi vilivyopigwa marufuku.

Alisema baada ya kukamata jengo hilo walipata taarifa kuwa kuna jengo jingine linalohifadhi vipodozi ambavyo vingi ni vilivyopigwa marufuku.

“Leo (jana) tumekamata jengo jingine lenye ghorofa tatu ambalo pia ghorofa zote zilikuwa na vipodozi ambavyo vingi ni vilivyopigwa marufuku,” alisema Alphonce.

Alisema TFDA itaendelea na msako ili kuhakikisha kuwa bidhaa zote zilizopigwa marufuku haziingizwi nchini.

Akizungumzia sakata hilo, Mkuu wa Kituo cha Polisi Msimbazi, Saeda Elisha, alisema muda umefika wa kuwakamata wafanyabiashara wakubwa wanaoingiza bidhaa zilizopigwa marufuku.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles