30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Tyra: Kuwa mama kunanifunza mengi

Tyra BanksNEW YORK, MAREKANI

MWANAMITINDO maarufu nchini Marekani, Tyra Banks, amesema tangu apate mtoto wake wa kwanza anaendelea kujifunza mengi kama mama wa familia.

Mrembo huyo alifanikiwa kupata mtoto wake wa kwanza wa kiume Januari mwaka huu na kumpa jina la York Banks na baba wa mtoto huyo anajulikana kwa jina la Erik.

“Nilikuwa nasikia sherehe za siku ya mama duniani, lakini mwaka huu nimekuwa na bahati kuwa miongoni mwa washerekeaji wa siku hiyo, ninaamini hadi sasa nimejifunza mengi kwa kipindi hiki.

“Kama nisingekuwa mama nadhani bado ningekuwa napitwa na mambo mengi, natumia nafasi hii kumshukuru mama yangu na mama wote kwa kusherehekea siku ya mama duniani, nawapenda sana,” aliandika Tyra.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles