27.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Tunda Man awataka wasanii kuwekeza

GLORY MLAY

MSANII wa muziki wa bongo fleva, Khalid Ramadhani, maarufu kwa jina la Tunda Man, amesema asilimia kubwa ya wasanii wanaotegemea muziki maisha yao ni mabovu, hivyo wanatakiwa kuwekeza.

Msanii huyo amesema, wapo wasanii ambao wanategemea muziki na maisha yao yapo vizuri, lakini wapo wachache wa aina hiyo.

“Hauwezi kutegemea muziki peke yake ukasema utakuwa na maisha maziri, msanii anayejitambua lazima atafute na biashara nyingine hata kama muziki unalipa lakini hauwezi kufikia yale malengo ambayo umeyapanga ni wachache sana wenye bahati hiyo.

“Hivyo msanii anatakiwa kujiongeza, wengi tunawaona walivyoishia katika maisha mabaya kutokana na wao kuwekeza kwenye muziki pekee bila kujua maisha ya baadae yatakuwaje,” alisema msanii huyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles