27 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Trump aanika sera zake za kigeni

Donald TrumpWASHINGTON, MAREKANI

MGOMBEA urais wa Chama cha Republican nchini Marekani, Donald Trump, ametoa hotuba muhimu kuhusu sera zake za kigeni huku kukiwa na wasiwasi kwamba hana uzoefu wala uelewa wa kutosha kuliongoza taifa hilo lenye nguvu zaidi duniani.

Katika hotuba hiyo, Trump aliahidi kuweka maslahi ya Wamarekani mbele akisema lengo la Marekani litakuwa amani na ufanisi na si vita na maangamizi.

Trump ambaye anapigiwa upatu kushinda tiketi ya chama cha Republican kutokana na kushinda katika majimbo mengi katika chaguzi za mchujo, alitumia muda mwingi katika hotuba yake kuhusu sera zake za kigeni kumponda Rais Barack Obama.

Alisema sera za kigeni za Obama ‘hazikuwa na mbele wala nyuma’ na zimewafanya washirika wa Marekani kupoteza imani na mahasimu kutoiheshimu.

Trump ameahidi kupambana dhidi ya itikadi kali za Kiislamu katika ukanda wa Mashariki ya Kati kwa kuimarisha udhibiti wa kikanda na pia ameahidi kuwa na uhusiano mzuri na Urusi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles