Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital
MSANII wa kizazi kipya anayeishi nchini Australia, Simorix The General ‘Jenerali’, ametamba kunogesha siku ya wapendanao (Valentine Day) na wimbo wake mpya Vaccine.
Simorix, ameiambia Mtanzania Digital kuwa wimbo huo wa Vaccine au Chanjo imepokelewa vizuri kwasababu ya ujumbe mzuri wa mapenzi kwenye msimu huu wa wapendanao.
“Vaccine imeanza kufanya vizuri hapa Australia katika kipindi hiki cha Valentine, ninaongelea penzi kama chanjo, naamini kila mtu ana mpenzi wake ambaye ana umuhimu mkubwa kwenye maisha yake na huu wimbo ni maalumu kwaajili yao,” amesema Simorix.