23.6 C
Dar es Salaam
Thursday, May 9, 2024

Contact us: [email protected]

Simorix The General anogesha Valentine na ‘Vaccine’

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

MSANII wa kizazi kipya anayeishi nchini Australia, Simorix The General ‘Jenerali’, ametamba kunogesha siku ya wapendanao (Valentine Day) na wimbo wake mpya Vaccine.

Simorix, ameiambia Mtanzania Digital kuwa wimbo huo wa Vaccine au Chanjo imepokelewa vizuri kwasababu ya ujumbe mzuri wa mapenzi kwenye msimu huu wa wapendanao.

“Vaccine imeanza kufanya vizuri hapa Australia katika kipindi hiki cha Valentine, ninaongelea penzi kama chanjo, naamini kila mtu ana mpenzi wake ambaye ana umuhimu mkubwa kwenye maisha yake na huu wimbo ni maalumu kwaajili yao,” amesema Simorix.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles