25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Simba dimbani kimya kimya kuwavaa El Merreikh

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Vinara wa kundi A, wawakilishi pekee wa ukanda wa Afrika mashariki katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Africa Simba almaarufu kama wekundu wa Msimbazi, leo hii itashuka katika dimba la Mkapa jijini Dar es Salaam kuwakabili El Merreikh kutoka Sudan.

Mchezo huo utacheza saa 10: 00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki, Simba wanaongoza kundi A wakiwa na alama 7, baada ya michezo mitatu.

Simba kama watapa ushindi leo au kutoka sare watakuwa wamejikita zaidi kileleni mwa kundi na kujihakikishia zaidi nafasi ya kucheza hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa Afrika

Michezo mingine itakayopigwa leo ni As Vita Club ya Jamhuri ya Kidemocracya Congo watakuwa wenyeji wa Al Ahly kutoka Misri.

Al Hilal vs Cr Belouizdad

Atletico Petroleos vs Kaizer Chiefs

Horoya Ac vs Wyadad Ac

Mamelodi Sundowns vs Tp Mezembe

Teungueth vs Mc Alger

Zamalek Sc vs Es Tunis.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles