24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

SADC: Marais Tshisekedi na Mokgweetsi wafanya mazungumzo

DRC, Kongo

Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na mwenzake wa Botswana, Eric Mokgweetsi Masisi wamekubali kuendelea kuzungumza kutafuta suluhisho kuhusu suala la wadhifa wa Katibu Mtendaji wa SADC.

Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na mwenzake wa Botswana Eric Mokgweetsi Masisi wamekubali kuendelea kuzungumza kutafuta suluhisho kuhusu suala la wadhifa wa Katibu Mtendaji wa jumuiya ya maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika-SADC.

Akiwa ziarani mjini Kinshasa jana Jumatatu, Rais Masisi alizungumza ana kwa ana na Tshisekedi. Viongozi hao wawili wamejadili maswala mengine kadhaa yakiwemo na kupambana na janga la Covid-19.

Botswana ilikuwa ya kwanza kuwasilisha ombi la kugombea nafasi ya Katibu mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC. Nafasi hiyo itakuwa wazi Agosti ijayo, lakini hii imekutana na changamoto baada ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo pia kutangaza pendekezo lake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles