25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

SHILOLE AWAJIBU WANAOIPONDA NDOA YAKE

Na ESTHER GEOR-DAR ES SALAAM


MSANII wa muziki nchini Tanzania, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, amefunguka na kusema wanaoiponda ndoa yake kwenye mitandao ya kijamii wana chuki binafsi.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Shilole alisema tangu afunge ndoa na mpenzi wake Uchebe, kumezagaa maneno ya majungu kitu ambacho hakiwezi kumkatisha tamaa na anaamini ndoa yake itadumu.

“Mfa maji aishi kutapatapa, ndoa yangu imewaumiza wengi wasionipenda, nimeona maneno ya kashfa na majungu wakinichafua, sasa mimi nasonga mbele na maisha yangu sina habari na mtu,” alisema Shilole.

Aliongeza kuwa familia yake imelipokea jambo hilo vizuri, licha ya kutokea migogoro ya hapa na pale lakini ni mambo ya kifamilia na wameyamaliza.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles