Abuja, Nigeria
Waziri wa Habari wa Nigeria, Lai Mohammed ameonya dhidi maandamano yaliyopangwa kufanyika huko Lekki jijini Lagos ambapo vikosi vya usalama viliwafyatulia risasi waaandamanaji Oktoba, mwaka jana.
Maandamano mapya, yaliyopewa jina la ‘Occupy Lekki toll gate’, yamepangwa kufanywa Jumamosi Waandaaji wanasema watagomea dhidi ya kufunguliwa tena kwa lango la ushuru.
Mohammed amesema serikali haitaruhusu maandamano mengine kufanyika.
Alisema wahalifu wanaweza kuvamia maandamano na kusababisha watu kupoteza maisha na uharibifu wa mali.
Amesema matangazo ya kuwataka watu kujitokeza kwenye maandamano yamekuwa yakisambazwa
Waziri aliongeza kuwa serikali ilikubaliana na matakwa ya awali na kuachiwa kwa waandamanaji waliokuwa wamekamatwa wakati wa wimbi la kwanza la maandamano na kuunda tume huru kutazama suala la ukatili wa polisi.