30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Salman Khan adai aliwahi kubaka

Salman KhanNEW DELHI, INDIA

NYOTA wa filamu nchini India, Salman Khan, ametakiwa kuomba radhi baada ya kuweka wazi kwamba aliwahi kubaka miaka ya nyuma.

Tume ya Taifa ya Kutetea Wanawake nchini humo (NCW), imesema msanii huyo anatakiwa kuomba radhi kutokana na kauli yake ya kudai kwamba aliwahi kubaka msichana lakini ilikuwa ni siri.

Katika maelezo yake kupitia akaunti yake ya Twitter, msanii huyo aliandika: ‘Katika maisha yangu niliwahi kubaka, lakini ilikuwa siri yangu, ilikuwa ni mwanafunzi mwaka 2012’ kutokana na maneno hayo NCW imemtaka msanii huyo kuomba radhi kwa kuwa ameikosea familia yake pamoja na wanawake wote.

“Salman Khan alichokiandika ni wazi kwamba amewakosea wanawake wote pamoja na familia yake, anachotakiwa kwa sasa ni kuomba radhi hata kama haikuwa kweli lakini ameweka wazi yeye mwenyewe,” waliandika NCW.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles