24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Rais aahidi kujenga gereza, raia wamcharukia

RAIS wa Misri, Abdul Fattah al-Sisi, amekosolewa vikali na raia wake baada ya kusema Serikali ina mpango wa kujenga gereza kubwa zaidi kuwahi kutokea katika historia ya nchi hiyo.

Wakosoaji wameuona mpango huo kuwa ni upuuzi kwani Serikali ilipaswa kuelekeza nguvu katika ujenzi wa hospitali, shule, makazi ya watu na miradi ya maji.

Mmoja kati ya wananchi hao, Areej Algana, amesema: “Nimewahi kusikia marais wakizungumzia miradi ya hospitali, viwanda na sayansi lakini si ujenzi wa gereza. Hii ni mara ya kwanza kusikia.”

Haytham Abokhalil ni raia mwingine wa Misri aliyeungana na Algana akisema: “Haya ya gereza yanakuja huku kukiwa na uhaba wa hospitali na shule…”

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles