25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Q BOY HUMTOI KWENYE MUZIKI, FASHENI

ALIYEWAHI kuwa msimamizi wa mwonekano wa Diamond Platnumz, ambaye pia ni msanii wa Bongo Fleva, Q Boy Msafi amesema alilazimika kwenda Afrika Kusini kusomea masuala ya fasheni na muziki kwa kuwa ni vitu vinavyoendana.

Akizungumza na Show Biz, Q Boy alisema mwanzoni alikuwa anapenda sana muziki na alifahamu ili kuwa mwanamuziki mzuri inakupasa kuwa na mwonekano mzuri wa mavazi ili sanaa yako ipokelewa vyema na jamii.

“Hapo ndiyo nikaingia ‘deep’ sana kusoma fasheni, nikasoma namna gani ya kumpendezesha mtu au msanii ili sanaa yake ipokelewe vizuri na jamii, huwezi kuutenganisha muziki na fasheni,” alisema Q Boy anayefanya vizuri na wimbo wake wa Karorero.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles