29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Petit kuhamasisha dansi Tanzania

Erick Mugisha (TUDARCo)

MWALIMU wa dansi nchini mwenye makazi yake Uholanzi, Petit Afro, amerudi Tanzania kwa ajili ya kuhamasisha vijana wenye vipaji vya kudansi.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Petit alisema baada ya kutoa elimu ya kudansi katika nchi mbalimbali barani Ulaya, sasa ameona bora arudi nyumbani kuwapa vijana elimu hiyo ambayo amekuwa akiwanufaisha wazungu zaidi ya miaka 10.

“Dansi ya kiafrika inapendwa sana na nchi za wenzetu, nimekuwa mwalimu wa kufundisha dansi huko Ulaya kwa zaidi ya miaka 10, sasa nimeona nirudi nyumbani kuwapa ninachowapa wazungu.

“Ninaamini wapo vijana wengi wenye vipaji hivyo huu ni wakati wao wa kuonesha walichonacho, wanaweza kujirekodi na kunitumia kwenye Instagram ili nione uwezekano wa kumsaidia,” alisema Petit.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles