NA CHRISTOPHER MSEKENA
MSANII anayekuja kwa kasi kwenye Bongo Fleva, Passo Music, amesema hajasainiwa kwenye lebo ya Danzak ila upambanaji wake ulimfutia staa huyo kumsaidia na kufanya wimbo wa pamoja unaoitwa Ipo.
Passo a.k.a Mwana Manzese, ameliambia MTANZANIA kuwa alikuwa anawasiliana kwa muda mrefu na Danzak ambaye mbali na muziki ni rubani wa ndege na katika mawasiliano yao aligundua ana kipaji kikubwa cha uimbaji na uandishi.
“Mimi nimepitia maisha magumu nimeshauza hadi mihogo lakini hii yote ilikuwa ni kutafuta njia ya kutokea, namshukuru sana Danzak kwa kunisaidia, hajanisaini kwenye lebo yake ila aliposikia maisha yangu akaguswa na tukafanya ngoma h