25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Panga pangua ya wabunge CCM

NAPE2Na Bakari Kimwanga, Dodoma

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekamilisha uteuzi wa wagombea ubunge wa majimbo na viti maalumu, huku baadhi ya wagombea walioshinda kwenye kura za maoni wakiachwa na kuchukuliwa walioshika nafasi ya pili na ya tatu.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema kukamilika kwa kazi hiyo kunatoa fursa kwa wana CCM kujipanga na kuhakikisha wanarudisha umoja na mshikamano ili chama kiweze kushinda uchaguzi katika ngazi zote.

Alisema pamoja na hali hiyo uteuzi huo wa wagombea wa nafasi mbalimbali umezingatia uwezo wa mwanachama  kukubalika kwa jamii pamoja na chama na kura za maoni haikuwa kigezo pekee cha uteuzi, ila vikao vya uteuzi huangalia sifa za ziada kwa mujibu wa utaratibu na kanuni za CCM.

Katika Jimbo la Handeni Vijijini, kikao hicho kimemteua Makamu Mwenyekiti wa UVCCM ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mufundi mkoani Iringa, Mboni Mhita aliyekuwa mshindi wa pili na kumwacha John Salu ambaye ushindi wake ulionekana kuwa na matatizo.

 

Kwa upande wa viti maalumu, Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Angella Kizigha, alijikuta akikubwa na kimbunga hicho kwa jina lake kukatwa, ambapo mshindi wa pili amekuwa wa kwanza na wa tatu amekuwa wa pili.

Mbali na huyo pia mtoto wa aliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, ambaye pia ni mgombea ubunge Jimbo la Ubungo Dk. Didas Masaburi naye amekumbwa na panga la NEC.

Mtoto huyo wa Masaburi, Juliana Masaburi, ambaye alishinda kura za maoni kupitia kundi la vijana akiwakilisha Mkoa wa Mara amekatwa na badala yake nafasi yake imechukuliwa na msanii maarufu wa Bongo Move, Irene Uwoya.

“Tumemaliza vizuri kazi ya uteuzi wa wagombea wa nafasi za ubunge wa majimbo viti maalumu, uwakilishi na uwakilishi viti maalumu. Kuna baadhi ya majimbo NEC tumefanya uteuzi kwa mtu wa pili na wa tatu na kuwateua kutokana na sababu mbalimbali.

“Na yapo baadhi tumerudia uchaguzi na hata kwingine kurudiwa kuhesabiwa kura upya ambapo hadi sasa hayo majimbo mchakato wake utakamilika Agosti 17, mwaka huu ambapo Kamati Kuu Maalumu itakutana na kufanya uteuzi wa mwisho,” alisema Nape.

Majimbo ambayo uteuzi umefanyika ni pamoja na Mkoa wa Arusha na majimbo yao katika mabano ni Philemon Mollel (Arusha Mjini), Dk. Wilbard Slaa Lorri (Karatu), Loy ole Sabaya (Arumeru Magharibi),  John Sakaya (JD) (Arumeru Mashariki), Dk. Stephen Kiruswa (Longido), Namelock Sokoine (Monduli) na William ole Nasha (Ngorongoro).

Dar es Salaam

Jimbo la Ukonga, kura zinarudiwa,  Ilala Mussa Zungu, Bonna Kaluwa (Segerea),  Abasi Mtemvu (Temeke), Dk. Faustine Ndugulile (Kigamboni), Issa Mangungu (Mbagala),  Kippi Warioba (Kawe), Dk. Didas Masaburi (Ubungo), Dk. Fenella Mukangala (Kibamba) pamoja na Iddi Azzan (Kinondoni).

Dodoma

Katika Mkoa wa Dodoma walioteuliwa  ni Juma Nkamia (Chemba), Omar Badwel (Bahi), George Simbachawene (Kibakwe), George Lubeleje (Mpwapwa), Livingstone Lusinde (Mtera), Antony Mavunde (Dodoma Mjini), huku Jimbo la Chilonwa kura zikirudiwa.

Wengine ni Job Ndugai (Kongwa), Sanda Edwin (Kondoa Mjini) na Dk. Ashatu Kijaji (Kondoa Vijijini).

Geita

Walioteuliwa ni Costantine Kanyansu (Geita Mjini), Joseph Kasheku (Geita Vijijini), Lolensia Bukwimba (Busanda), Augustino  Massele (Mbogwe), Dotto Biteko (Bukombe) huku mrithi wa Dk.John Magufuli ambaye kwa sasa ni mgombea urais wa CCM ni  Dk. Medard Kalemani (Chato) na Hussein Amar (Nyangwale).

Kagera

Walioteuliwa ni Balozi Khamis Kagasheki (Bukoba Mjini), Jasson Rweikiza (Bukoba Vijijini), Osca Mkasa (Biharamulo), Innocent  Bashungwa (Karagwe), Innocent Bilakwate (Kyerwa), Charles Mwijage (Muleba Kaskazini), Profesa Anna Tibaijuka  (Muleba Kusini), Dk. Diodorus Kamala (Nkenge) na Alex Gashaza (Ngara).

Iringa

Kwa upande wa Mkoa wa Iringa ni Fredrick Mwakalebela (Iringa Mjini), Williaam Lukuvi (Isimani), Godfrey Mgimwa (Kalenga), Kilolo (Kura zinarudiwa), Mahmoud Mgimwa (Mufindi Kaskazini),  Mendrad Kigola (Mufindi Kusini) na Cosato Chumi (Mafinga Mjini).

Katavi

Walioteuliwa ni Sebastian Kapufi (Mpanda Mjini), Mos Kakoso (Mpanda Vijijini), Issack Kamwele (Katavi), Richard Mbogo (Nsimbo) na Dk. Pudenciana Kikwembe  (Kavuu).

Kigoma

Walioteuliwa ni Christopher Chiza (Buyungu),  Atashasta Nditye ambaye alikuwa mshindi wa tatu (Muhambwe), Daniel Nsanzugwanko (Kasulu Mjini), Augustino Holle (Kasulu Vijijini), Albert Ntabaliba (Manyovu), Amani Kabourou (Kigoma Mjini), Peter Serukamba (Kigoma Kaskazini),   Hasna Mwilima (Kigoma Kusini).

Kilimanjaro

Katika uteuzi huo NEC imewateua, Danstan Mallya (Hai), Aggrey Mwanri (Siha), Davis Mosha  (Moshi Mjini), Profesa Jumanne Maghembe (Mwanga),        Anne Kilango Malecela (Same Mashiriki),  David Mathayo (Same Magharibi), Dk. Cyril Chami (Moshi Vijijini),       Innocent  Shirima (Vunjo), Sanje Colman (Rombo).

Lindi              

Walioteuliwa kuwania ubunge kupitia CCM ni Kassim Majaliwa (Ruangwa), Faith Mitambo (Liwale),Hassan Masala (Nachingwea) Nape Nnauye (Mtama), Said Mtanda (Mchinga), Hassan Kaunje (Lindi Mjini), Hasnain Dewji (Kilwa Kusini), Murtaza Mangungu (Kilwa Kaskazini).

Manyara

Hali ilikuwa tofauti kwa wagombea wa majimbo ya Babati Mjini na Vijijini ambapo wajumbe wa NEC waliponga kukatwa na wagombea hao na kutaka warejeshwe katika kinyng’anyiro ambapo nafuu ikapatikana kwao  Kisyeri Chambiri (Babati Mjini),  Jittu Vrajilal Son (Babati Vijijini), Dk. Mary Nagu (Hanang’), Kiteto (Litaamuliwa na Kikao Kijacho cha Kamati Kuu), Zacharia Issaay (Mbulu Mjini), Fratei Massay   (Mbulu Vijijini), Christopher Ole Sendeka(Simanjiro).

Mbeya

Sambwee Shitambala (Mbeya Mjini), Oran Njeza (Mbeya Vijijini), Haroon Mullah(Mbarali), Sauli Amon  (Rungwe), Atupele Mwakibete (Busokelo),   Janeth Mbene (Ileje), Weston Zambi (Mbozi), Ngailonga Kasunga (Vwawa), Luca Siyame (Momba), Frank Mastara Sichalwe (Tunduma), Victor Mwambalaswa (Lupa) na Philip Mulugo(Songwe).

Mbali na hilo pia alisema katika jimbo la Singida Mashariki ambalo linaongozwa na Tundu Lissu (Chadema), matokeo yake yamefutwa na mchakato utaanza upya ndani ya CCM kwa wagombea kuchukua fomu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles