23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

NEY WA MITEGO: DIAMOND, KIBA HAWANITISHI

Na MOHAMED KASSARA- DAR ES SALAAM

MKALI wa muziki wa hip hop Tanzania, Emmanuel Elibariki ‘Ney wa Mitego’, amesema hazimwi na bifu la Dimoand na Ali Kiba, huku akiweka wazi kuwa yeye hana mpinzani hapa nchini katika aina ya muziki anaoufanya.

Akizungumza jana alipotembelea ofisi za Kampuni ya New Habari 2006 Ltd, inayochapisha magazeti ya Mtanzania, Bingwa, Rai na Dimba, Ney alisema ushindani uliopo kati yao haumtishi kuachia nyimbo zake kwa kuwa hajawahi kufunikwa.

Rapa huyo anayetamba na video ya wimbo wake mpya wa ‘Makuzi’, alisema hawezi kufunikwa kutokana na ubunifu wake.

“Mimi sina mpinzani katika muziki wangu ndio maana sijahofia kutoa wimbo kwenye kipindi hiki ambacho Diamond na Kiba wapo kwenye upinzani mkubwa, ninaamini upinzani wao unachangamsha muziki, lakini hawanitishi,” alisema Ney.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles