25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Ney kumwokoa mama mtoto wake

NEY WA MITEGONA BEATRICE KAIZA

MSANII  wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Ney wa Mitego’, amesema yupo tayari kumtolea dhamana mpenzi wake wa zamani, Siwema ambaye amehukumiwa kwenda jela miaka miwili kwa kosa la kumtukana shabiki kwenye mtandao wa kijamii.

Ney na Siwema walifanikiwa kukaa kwenye uhusiano kwa kipindi kirefu na kufanikiwa kupata mtoto ambaye walimpa jina la Curtis kabla hawajatengana.

Akizungumza na MTANZANIA, Ney wa Mitego alisema: “Mimi na Siwema kwa sasa si wapenzi kila mtu na maisha yake lakini ni mama wa mtoto wangu, niliposikia kuwa amehukumiwa jela miaka miwili sikuwa sawa kabisa kwa sasa napambana kile nitakachoweza kuangalia kama kuna uwezekano wa kumpa msaada.

“Kuna vitu nafikiria kuvifanya ili kujaribu kumsaidia, yeye ni mzazi mwenzangu na tulikaa muda mrefu kwa sasa si mpenzi wangu lakini nawaza kumsaidia kumtolea dhamana,” alisema Ney wa Mitego.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles