23.3 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Mtoto wa Mungai aahidi neema Mafinga

OTH_1303Na Gustaph Haule, Mafinga

MGOMBEA Ubunge wa Chadema   Mafinga Mjini, William Mungai, amewaomba wananchi  kumchagua   aweze kuleta mabadiliko ya  maendeleo.

Alisema amejitosa kugombea nafasi hiyo kwa lengo la kuwaletea maendeleo wananchi katika sekta mbalimbali kwa kukabaliana na changamoto zilizopo ikiwamo afya, maji, viwanda, miundombinu, elimu   na kuimarisha uchumi kupitia taasisi za  benki.

Mtoto huyo wa Mungai alisema jimbo hilo limekuwa mstari wa mbele katika kuchangia mapato ya serikali kwa kushika nafasi ya pili mbele ya Temeke hivyo hakuna sababu ya kurudi nyuma katika maendeleo.

Alisema  akiwa mbunge atahakikisha anajenga viwanda vidogo na vya kati  mazao ya Mafinga yasindikwe tofauti na ilivyo sasa.

“Nitashirikiana na halmashauri yangu kutenga maeneo ya uwekezaji   na kuitangaza Wilaya ya Mufundi na jimbo lake la Mafinga kupitia Taasisi za  benki ili nazo ziwekeze kwa faida ya wanaMafinga lakini pia Mafinga lazima ijenge viwanda vya mbao vitakavyosaidia kuongeza thamani ya mbao wanazozalisha,”alisema Mungai.

Akizungumzia sekta ya elimu, Mungai alisema   yupo tayari kufuata sera ya Chadema ya kufuta michango yote shuleni   wanafunzi wake wasome bila ya usumbufu  na hivyo kufanya idadi ya wataalamu waongezeke.

Kwa kufanya hivyo baada ya miaka mitano kutakuwa na idadi kubwa ya wananchi wa Mafinga waliopata elimu, alisema.

Alisema   atahakikisha changamoto za  elimu zilizopo   Mafinga kama vile ukosefu wa madawati, nyumba za walimu    na kuboresha maslahi yao anazifanya kwa kiwango kikubwa  kuwapa molari walimu kufundisha kwa bidii.

Alisema hakuna jambo litakaloshindikana katika uongozi wake.

Hata hivyo, alisema ili kukabiliana na changamoto hizo ni lazima wananchi wa   Mafinga wajitokeze kwa ukamilifu kumchagua katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu   aweze kuleta mabadiliko.

Aliwataka waache kusikiliza propaganda za wapinzani wanaotaka kuchukua madaraka kwa mabavu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles