24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Minaj atembelea hospitali ya watoto Philadelphia

nicki-minajPHILADELPHIA, Marekani

NYOTA wa muziki wa Hip Hop kwa wanawake nchini Marekani, Nick Minaj, juzi aliwatembelea watoto katika hospitali ya Philadelphia nchini Marekani.

Kupitia akaunti yake ya Instagram, Minaj aliandika kuwa anajisikia furaha kutembelea hospitali hiyo na kufanya mazungumzo na watoto hao.

“Ninaamini watoto wamepata faraja kubwa kuniona na mimi nimejisikia kuwa na furaha kubwa kwa kuwa nimewaombea kwa Mungu ili wapone haraka.

“Nilikuwa na furaha kubwa kuwaona watoto wakiwa na furaha baada ya kuniona, hii inaweza kuwapa afya njema kutokana na aina ya magonjwa yao,” alisema Minaj.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles