PARIS, Ufaransa
BAADA ya Rais wa Barcelona, Joan Laporta, kusema kuna siku Lionel Messi atarejea klabuni hapo, imeripotiwa kuwa staa huyo wa PSG hafikirii suala hilo.
Laporta alisema anaaamini Messi na nyota mwingine wa zamani wa timu hiyo, Andres Iniesta, watarudi Camp Nou kama alivyofanya beki mkongwe, Dani Alves.
Kauli yake hiyo iliungwa mkono na kocha mpya, Xavi, aliyesema anatamani kuona akifanya kazi na wawili hao aliowahi kucheza nao Barcelona misimu kadhaa iliyopita.
Hata hivyo, kwa mujibu wa taarifa kutoka Ufaransa, Messi ameelekeza akili yake katika kuiwezesha PSG kutwaa mataji na haoni kama kuna uwezekano wa kuichezea Barca katika siku za usoni.