LOS ANGELES, Marekani
MCHUMBA wa aliyekuwa mwandishi wa habari maarufu wa Saudi Arabia, Jamal Khashoggi, amemwandikia barua staa wa muziki wa Pop, Justin Bieber, akimwomba kutokwenda kufanya ‘shoo’ katika taifa hilo la Kiarabu.
Bieber anatarajiwa kuingia Saudi mwezi ujao lakini bibiye Hatice Cengiz amemtaka kubadili uamuzi ili uwe ni ujumbe dhidi ya Serikali ya nchi hiyo iliyohusika katika kifo cha mpenzi wake, Khashoggi.
Khashoggi aliuawa mwaka 2018 akiwa jijini Istanbul, Uturuki, huku ikielezwa kuwa ulikuwa ni mpango wa Serikali ya Saudi kwa kuwa alikuwa akiikosoa mara kwa mara.
Katika ujumbe wake kwa Bieber, Hatice aliyekwishavishwa pete na Khashoggi, amesema: “Usiende kuwaimbia watu waliohusika kumuua mpenzi wangu, Jamal.”