26.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Majuto awataka wasanii kuelimisha jamii

king_majutoNA THERESIA GASPER

MCHEKESHAJI mkongwe nchini, Amri Athumani ‘King Majuto’, amefunguka na kudai kwamba kuna baadhi ya wasanii wa filamu wanafanya kazi zao bila ya kuwa na lengo la kuelimisha jamii zinazowazunguka.

Msanii huyo amedai kwamba, wasanii wengi wapo kwa ajili ya kufurahisha watu lakini wanasahau kwamba wanatakiwa kuelimisha jamii kwa kuwa wao ni kioo cha jamii.

“Ukiangalia filamu zangu nakuwa nachekesha lakini nafundisha, ila kuna wasanii wengine kazi yao kubwa ni kuchekesha katika kila filamu lakini hawatumii muda wao kwa ajili ya kuelimisha,” alisema Majuto.

Mkongwe huyo amekuwa na idadi kubwa ya mashabiki kutokana na uwezo wake wa uigizaji.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles