23.6 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Madrid waachana na Mbappe

MADRID, Hispania

UONGOZI wa Real Madrid umeona ni bora kuachana na mpango wa kumchukua mshambuliaji wa PSG na timu ya Taifa ya Ufaransa, Kylian Mbappe, kupitia usajili wa Januari, mwakani.

Uamuzi wao huo umekuja baada ya kukubaliana wasubiri mwishoni mwa msimu huu kwa kuwa Mbappe atakuwa mchezaji huru.

Kwa kuwa Mbappe atakuwa na mkataba kufikia Januari, Madrid watalazimika kulipa kiasi kikubwa cha fedha, ambacho hakitakuwepo majira ya kiangazi kwa sababu atakuwa amemaliza mkataba wake na PSG.

Madrid wamejaribu mara kadhaa kuinasa saini ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 na miezi michache iliyopita Rais wa klabu hiyo ya La Liga, Florentino Perez, alisema atamchukua ifikapo Januari.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles