31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Madiwani wapiga kura ya kutokuwa na imani na Mike Sonko

Nairobi, Kenya

Madiwani 88 kati ya 122 wa kaunti ya Nairobi wamepiga kura ya kutokuwa na imani na Gavana wa Nairobi, Mike Sonko hii ni idadi ambayo imepitisha kiwango cha theluthi tatu kumuondoa gavana aliyemadarakani.

Kwa mujibu wa taarifa, kitakacho fuata sasa ni wasilisho la matokeo hayo mbele ya bunge la Seneti ambapo hatma ya gavana wa Nairobin imo mikononi mwao.

Awali, gavana huyo alikuwa ametuma ombi katika mahakama kuu kusitisha hatua ya kuondolewa kwake akisema kwamba ni kinyume cha sheria na kinyume na katiba vilevile.

Je ni mwisho wa ugavana wake?

Kwa gavana ambaye kipindi fulani alikuwa mwenye nguvu na utawala wa aina yake, ikiwa bunge la seneti litadumisha matokeo ya kura ya kutokuwa na imani naye yaliyowasilishwa na bunge la kaunti, kitakachofuata itakuwa ni kuandaliwa kwa uchaguzi mpya katika kaunti hiyo kumchagua gavana na naibu wake na kutamatisha utawala wa gavana huyo aliyekuwa na madoido ya kipekee.

Na pia ikumbukwe, hadi anapigiwa kura ya kutokuwa na imani naye, Sonko alikuwa hana naibu gavana.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles