24 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Maabara zawavutia wanafunzi masomo

NA SAMWEL MWANGA

WANAFUNZI wa  Shule ya Sekondari Mwamishali  wilayani Meatu  wameanza kusoma masomo ya sayansi kwa vitendo huku wakipongeza uamuzi wa Rais Kikwete wa kuagiza ujenzi wa maabara kwa shule zote za kata.

Pongezi hiyo zilitolewa jana   ba  Mariamu Mwirabi,  mbele ya Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru, Juma Khatib Chum  alipofungua
vyumba vitatu vya maabara katika shule hiyo.

Mwirabi alisema kabla ya agizo hilo walikuwa wakisoma masomo ya sayansi kwa kutumia picha na michoro hali ambayo iliwafanya wanafunzi  wengi kuyakimbia masomo hayo.

“Kwanza tunapenda kumshukuru rais wetu kwa kuona umuhimu wa kutoa agizo hili kwa sasa imetusaidia kwa vile awali baadhi yetu walikuwa wakikimbia masomo  ya sayansi lakini baada ya kuanza kusoma kwa vitendo masomo yanaonekana rahisi,” alisema .

Walisema  awali shule za kata zilikuwa zikidharauliwa na baadhi ya watu kwa kukosa ubora lakini baada ya kujengwa maabara shule hizo zimeanza kuonyesha  ubora wake kwa kufaulu wanafunzi wengi.

Naye  Chum alisema dhamira ya serikali kusisitiza ujenzi huo ni kuongeza wataalamu wakiwamo wahandisi   na madaktari.

“Dhamira ya serikali  kujenga vyumba vitatu vya maabara kwa ajili ya kemia, bailojia na hisabati   tuweze kupata wataalamu wa kutosha katika fani mbalimbali za sayansi zikiwamo za kupata madaktari na wahandisi hivyo ni vizuri tukaitumia fursa hii kutoa elimu bora,” alisema.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles